FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

CHIDY BENZ KUGEUKIA UJASILIAMALI




IKIWA ni takribani muhongo mmoja tokea msanii wa Bongo Fleva Rasheed Makwiro, Chiddy Benz kutambulika katika tasnia ya muziki wa Bongo Fleva, staa huyo amefunguka kujaribu kete yake katika biashara ikiwa alikuwa akifanya muziki kama biashara japo si biashara rasmi.

Akipiga stori na LAJIJI kwa njia ya simu Chiddy amesema kwa sasa anajikita katika baishara ya uuzaji wa mkaa. Yawezekana Chidd amefanya tafiti ya kutosha na kuja na biashara hiyo kwani mjini zipo fursa nyingi lakini yeye amechangua kuja na aina hiyo ya biashara.

“Mimi ni mwana  Dar es Salaam, najua wana Dar es salaam wanahitaji nini, nimekulia Ilala pale najua jambo linalohitajika kwa kiasi kikubwa kwa matumizi, wasanii wengi wanafungua maduka ya nguo. Kuvaa siku hizi ni chaguo tu wala sio lazima. Kwanza wajanja wote wanatafuta hela wala sio ishu za kuvaa vaa” alisema Chiddy

Watanzania wanampuuzia msanii huyo kwa kudhani huwenda ni athari za matumizi ya dawa  za kulevya ndiyo yanamuendesha kiasi cha kuwa hivyo, LAJIJI limezungumza naye na kubaini kuwa jamaa anajielewa na anaelewa nini anafanya.
Ikumbukwe Chiddy Benzy amewahi kutiwa nguvuni mara kadhaa jijini Dra es Salaam  na mikoa ya jirani kwa makosa mbalimbali ikiwemo kudaiwa kukutwa na dawa za kulevya.