FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

WASANII BWANA WAAISHIWI NA MAMBO

Irene Paul awaasa mastaa kuacha kujichumbua




Muigizaji wa Bongo Movie Irene Paul amewaasa   Mastaa wenzake kuacha kujichumbua na wabaki katika uhalisia wake kwani licha ya kupata madhara makubwa baadaye  pia hugharimu gharama kubwa ambapo matokea yake ni hatari kiafya.
Msanii huyo alijitolea mfano kwake yeye kwa kuonekana na rangi yake kuwa asili na yakuvutia na kusema kuwa ni gharama ndogo sana ambayo anatumia kwa kununua vitu vya kawaida ambavyo vinaonesha ngozi yake kuwa asili kila siku.

Ukitaka kuniangalia kuanzia kichwani hadi ngozi yangu situmii gharama hata kidogo, naamini mastaa wengine wakiamua kuwa jinsi walivyo watapendeza na wataepuka gharama ambazo si za muhimu“ alisema Irene Paulo
Hata hivyo msanii huyo anasema kuwa mastaa hao wamekuwa wakijichubua kwa kutafuta kuoneka kuwa na mvuto na kupendeza  lakini wengi wao hawako hivyo licha yakutaka kuonekana hivyo kunamadhara makubwa sana
Wakati msanii huyo akiwataka mastaa kutojichumbua msanii wa muziki 

Ray­mond Mwakyusa ‘Rayvanny’ alikaliliwa na wanazengo kuwa anajichumbua kitendo ambacho amekanusha na kusema siyo kweli.
“Jamani mimi hizo tabia nimezianza lini tena? Yaani walimwengu hawakosagi cha kusema, unajua kuna picha ambazo zikitupiwa mtandao­ni naonekana mweupe sana na nyingine zinakuwa zime­toka vibaya, hapo watu ndiyo huanza kusema nimejichibua, kitu ambacho siyo kweli,” alisema Rayvanny.

LAJIJI halikuishia hapo lilifanya utafiti zaidi ili kujua madhara makubwa yatokanayo na kujichumbua kwa kutumia vipondozi ambavyo ni hatali kwa afya .
 Katika bidhaa zinazotumika kujichubua, kuna kemikali za aina mbili. Ambayo ni ‘Hydroquinone’ na ‘Mercury’

Hydroquinone kemikali hii ni sumu kali, ambayo hutumika kwa ajili ya kuchapisha picha na kutengeneza bidhaa za mpira. pia kama kisaidizi katika kutengeneza rangi za nywele. Mercury nayo ni kemikali ya sumu inayoweza kuuzwa katika maduka ya madawa

Dkt. Elizabeth Kilili, ni mtaalamu na Mkurugenzi Mtendaji wa Grace Product Limited ambaye ameainisha madhara yatokanayo na matumizi ya vipodozi maarufu kama kujichumbua kitendo ambacho ni hatali sana.
“Kujijumbua kunahatali kubwa sana ikiwa ni pamoja na kupata kansa ya ngozi, kuzeeka mapema,kupata watoto wenye kasoro, mishipa ya fahamu,figo, kupungua kwa uzito na kupelekea athari za kuvunjika mifupa.Madhara haya huoneka mara moja na kadri mtu anavyozidi kutumia mkorogo kung'arisha ngozi yake.

Dkt Kilili anaendelea kwa kutoa ushauri wa kuepukana na madhara ya kujichubua huku akishauri matumizi ya bidhaa za asili zisizokuwa na madhara, ikiwemo kutumia vipodozi vilivyopitishwa na Mamalaka ya Chakula na Dawa (TFDA) pamoja na kupata ushauri kwa wataalamu juu ya afya na magonjwa ya vipodozi ikiwemo kujikinga na madhara yanayoweza kusambabisha athari katika mwili wako.

Ukweli ni kwamba wapo mastaa wengi ambao wanajichumbua kitendeo ambacho kinasababisha baadhi ya jamii kuiga kwa kuona muonekano ambao si halisi hivyo kuna hitaji kwa namna moja au nyingine kila mmoja kujitasumini na kuacha kabsa kwani ni hatali sana



Lady Gaga aweka histori kushinda tuzo za Oscar 2109







Kupitia tuzo kubwa duniani za Filamu za Oscar 2019 ambazo zilifanyika Los Angeles Marekani, ambapo ilihusihwa na utowaji wa tuzo kwa washindi mbalimbali mwanamuziki nchini humo Lady Gaga ameweka historia ya kipekee katika maisha yake.

Gaga ameibukuka kidedea na kujinyakulia ushindi ambao umempa tuzo ya kipekee kuwa msanii bora kupitia wimbo wake uitwao ‘Shallow’ na hii ikiwa ni mara ya kwanza kwake tangu tuzo hizo zianzishwe.

Lady Gaga anaingia kwenye orodha ya wasanii wa muziki ambao walishawahi kushinda tuzo hizo, kama Cher, Jennifer Hudson, The Beatles, Prince, Elton John, Adele na wengine kitendo ambacho kinaleta hamasa kubwa ya kuzidi kufanya vizuri katika muziki

Utoaji wa tuzo kwa washindi ambao kwa namna moja au nyingine wanafanya vizuri katika kazi yao ya kimuziki ni moja ya msanii husika kumpa uwezo wa kufikilia zaidi kwa kufanya muziki ambao ni bora na wenye kufuata taratibu husika

Hata hivyo kupitia tuzo hizo kwa upande mwingine Washirika wawili katika filamu ya ‘Black Panther’ ambao ni Ruth Carter na Hannah Beachler alishinda tuzo ya ubunifu wa filamu kwa pamoja na mshindi mwingine Jay Hart.  wameweka historia katika tuzo hizo kwa kuibuka washindi wa kwanza weusi katika vitengo walivyoshinda.
 “Huenda Marvel imeunda shujaa wa kwanza mtu mweusi lakini kwa kutumia mavazi ya ubunifu tulimgeuza kuwa mfalme wa Afrika.” Alisema Hannah Beachler

Tukiachilia mbali na tuzo hizo zilizotolewa nchini humo Tanzania kupitia Bodi ya Filamu na Sinema Zetu International Film Festival Award (SZIFF) 2019 ilitoa tuzo kwa washindi mbalimbali kama vile mwanamuziki bora, muingizaji bora, mchekeshaji bora,  na nyingine ambapo wahusika walipewa tuzo maalumu ambazo ni moja ya historia katika maisha yao.






Sina mpango tena na Bongo Fleva; Pretty Kind








Aliyekuwa mwanamuziki wa Bongo Fleva Suzani Michael ‘Pretty Kind’ ametanganza rasmi kuachana na muziki wa kidunia na kuamua kuanza kuimba nyimbo za Injili ambapo anaona kuwa ni sehemu sahihi kwa sasa

Msanii  huyo anongeza kuwa ameacha kuimba muziki huo kwa sababu ameamua kuachana na mambo ya kidunia ambayo hayana faida yeyote katika maisha yake na kugeukia rasmi katika kujikita kuimba nyimbo za injili kwani  kwa sasa anasema kuwa ameokoka natangu afanye uamuzi huo moyo wake umekuwa wa furaha sana

“Tangu nimeokoka maisha yangu yamekuwa ya furaha mno na nina amani moyoni tofauti na nilivyokuwa naendekeza maisha ya kidunia hivyo ili kudhihirisha furaha aliyonipa Mungu, sasa ninaanza kuimba nyimbo za Injili ili ziwe ushuhuda wa kuwabadili na wengine“. Alisema suzan

Hata hivyo alijihakikishia kusimama imara katika kuhakikisha kwamba anazikabiri changamoto ambazo zitakazotokea sababu kumpokea Mungu kuwa mwokozi wa maisha yako  lazima muda mwingine  upate majalibu hata hivyo kwa uwezo wa Roho Mtakatifu ambaye yeye ni mlizni katika maisha ya mwanadamu, kamwe yeye hawezi kuanguka .

Ikubukwe kwamba kumekuwepo na baadhi ya wasanii kuacha muziki wa Bongo Fleva maarufu kama muziki wa kiduni na kugeukia upande wa pili wa nyimbo za injili madharani  Goodluck Gozbert akiwa ni moja wasanii wa aina hiyo.