FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

HAROMINIZE AMUANDIKIA UJUMBE MZITO RICH MAVOKO


Msanii wa Bongo Fleva, Rajabu Abdul ‘Harmonize’ amemuandika ujumbe mzito msanii mwezake Rich Mavoko, adai kuwa anafahamu machungu anayopitia kwa sasa hadi kupelekea ukimya wake, ahoji wanaofurahia kupotea kwake wananufaika na kipi hasa.

Harmonize ameandika ujumbe huo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo pia umeibua hisa kali kwa baadhi ya watu
“Familia ngapi zipo nyuma ya Rich Mavoko ? na zinamtegemea yeye kwakila jambo hasa hili la kupata mkate wa kilasiku vip kuhusu ndoto za familia hizo na zinaishije katika wakati huu?
Ndoto ngapi za wasani ambao wanategemea kuzifikia hizo ndoto kupitia Mavoco ? na nyuma ya hao wasanii kuna familia nyengine pia.

Je? maumivu malalamiko ya wazazi wake hasa mama mzazi ambae ndio kama roho yake! ushajiuliza ni kauli ngapi za uchungu anazitoa ambazo zinaweza kumpata kila anaefurahishwa na hili kwa makusudi ?

Maana mzazi wa mwenzio ni wako pia laana yake haishindwi kukupata ! la mwisho kabisa mgeukie mwenzio anaefurahia na kuifanya hii kuwa ni habari njema kwake ya kumfanya atembee kifua mbele na hata kuandika mtandaoni kwa furaha Mavoco kapotea muulize anafaidika na nini ?.

Mungu anasababu na maana yake bro Richi Mavoco kama mdogoako nakuombea najua ukimya wako unamaana kubwa sanaa ndani yako ninachojua ni kujiweka sawa na kutuletea kazi zingine tunakupenda na tunakuombea mungu akufanyie wepesi.! Let’s go bro mdogoako rafiki yako nipo hapa muda wowote! Ramadan Kareem.” Aliandika Harmonize

Ikumbukwe kwamba toka Desemba 31, 2019, Mavoko hajaposti chochote kile kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii wala kutoa wimbo mpya au kushirikishwa na msanii mwingine.





HUSSEIN MACHOZI AWEKA WAZI JAMBO HILI



Msanii wa Bongo Fleva, Hussein Rashid ‘Hussein Machozi’ ambaye amekita makazi yake nchini Italia kwa muda kwasababu ya covid 19 ameweka wazi hali ya sasa nchini humo.

Hussein alisema kuwa kwa sasa mashariti ya kukaa ndani yamelegezwa hivyo watu wanatoka nje licha ya kuwekewa mipaka.

“Kwa sasa tunaweza kutoka nje tukazunguka lakini pia kuna mipaka tumewekewa kwa mfano huwezi kutoka Morogoro ukaenda Dar Es salaam yaani umetoka nje ya nyumba yako unaweza kwenda Kipunguni, Kariakoo hauruhusiwi kuvuka mkoa kwa mkoa
Lakini jambo ambalo tunafurahi kwanza vifo vimepungua siyo kama vilivyokuwa mwanzo na kitu ambacho kimesababisha vifo kupungua ni kukaa ndani na kusikiliza maelekezo asikwambie mtu uzima uko ndani” alisema Hussein Machozi.  

Aidha aliongeza kuwa “baadhi ya vitu vimefunguliwa ikiwemo wajenzi wanaojenga, tunaomba tu Mungu hali izidi kupungua ili watu tufanye kazi zetu kama kawaida kwasababu ni kweli huu ugonjwa umekata hesabau nyingi sana kwa hivyo tuombeane kote Ulimwenguni kwasababu huu ungonjwa siyo wa Italia au China pekee yake”.






R.KELLY MBIONI KUTOKA GEREZANI



Msanii wa muziki nchini Marekani, Robert Sylvester Kelly ‘R Kelly’ huwenda akaanza kuonekana akiwa huru kwa muda fulani, hii ni baada ya kugundulika anaugua kisukari (diabetes) kwa muda mrefu huku juhudi za kutoka kwake zikifanywa na wakili wake, Steven Greenberg.

Sasa maombi haya ni ya muda mrefu kwa wakili huyo juu ya jaji wa kesi zinazo muandama mkongwe huyo na ikimchukua muda mrefu kushughulikia kesi hiyo kutokana na makosa ya jinai yanayo muandama mteja wake.

Hofu kubwa ni kuwa kinga yake ya mwili imepungua hivyo itamfanya kushambuliwa na maambukizi ya Corona hasa akiwa gerezani kwani hakuna njia sahihi ya kujikinga ukizingatia kuna msongamano wa wafungwa.

Itakumbukwa, R.kelly anashikiliwa kwa makosa ya unyanyasaji wa kijinsia (Ubakaji), pia kufunga ndoa na mwanamuziki Aaliya huku akiwa na umri chini ya miaka 18.





DIAMOND PLATNUMZ AANZA KUTEKELEZA AHADI YAKE


Msanii wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametoa msaada wa kodi ya pango kwa watu 57 ambao ni wajane, walemavu pamoja na wasiojiweza.

Msaada huo ni waawamu ya kwanza katika ile dhamira yake ya kusaidia kodi ya pango kwa kaya 500 nchini zilizoathirika kiuchumi na janga la mlipuko wa virusi vya Corona.

Kufuatia jambo hilo, familia zilizobakia kwenye orodha ya kaya 500 ni 443 ambapo mchakato unaendelea kwa ajili ya kuzipata kaya za wajane, walemavu na wasiojeweza.