FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

USHAURI WA TECHNOLOGY NAMNA YA KUISHI KATIKA KIPINDI HIKI CHA CHANGAMOTO KWA BAADHI YA WATU


Hali ngumu inapotokea yaani  (Crisis) mara nyingi huwa inatoa matokea ya kutengeneza makundi mawili, kundi la kwanza ni watu ambao wanashindwa (Fail) katika kipindi hiki kigumu watu hawa hupoteza kazi, mitaji,biashara,fedha,  na mambo mengine yakwao huenda tofauti .
Lakini katika huu wakati kuna watu wataibuka ambao wanaitwa washindi au watu wanao pata (gain) kwa maneno mengine hakuna kupoteza kwa ujumla kwa sababu kuna baadhi watapa na wengine watapoteza.

Kwahiyo hakuna (Crisis) au mgogoro, jambo fulani gumu linapotokea linalokuwa halina kitu ndani yake  matatizo yanapokuja kunakuwa na makusudi fulani yanakuwepo ambayo yamejificha ndani ya ule mgogoro kwahiyo tunapojifunza masuala ya kifedha lazima tufahamu kwamba hali kama hii inapotokea huwa inakuwa imebeba nini? Kuna kitu fulani kimejificha kwahiyo tusichukulie tu kama jambo la kawaida ili mbeleni isije kutuathili pakubwa.

kusudi la kuwepo kwa changamoto kama ya aina hii
Kusudi la kwanza la hali ngumu inapokuwa imetokea moja wapo ni kudhihilisha udhaifu ambao upo katika maeneo mbalmbali, udhaifu huu unaweza kuanzia kwenye nchi kwa mfano mfumo ya nchi, mfumo wa kifamilia ,mfumo ya kitaasi.

Kabla ya changamoto kubwa kutokea kila mtu huwa anakuwa hodari (stable), maisha ya kila mtu huwa sawa sawa, kila mtu hujiona kuwa hawezi kuyumba au kuteteleka lakini inapotokea wakati kama huu ndipo haya mambo yanaanza kujionesha, udhaifu huanza kuonekana. Eneo la kwanza kabisa ni katika mfumo wa kifedha kabla ya wakati huu mgumu kila mtu alikuwa anajiona yuko salama mambo yake yako vizuri hawezi kuteteleka kwa namna moja au nyingine ,

baadhi ya watu walikuwa wakiona biashara zao ziko vizuri pia vipato vyao lakini jambo kama hili lilipotokea limedhihilisha kwamba kumbe kuna watu mifumo yao ya kifedha haiko imara au dhabiti wameshindwa kuingiza tena fedha waliokuwa wanaishi maisha mazuri baadhi yao maisha yamebadilika pakubwa wameporomoka sana kutoka juu mpaka chini.

Kwahiyo hii inadhihilisha na kuchimbua udhaifu tulionao na ni muhimu kuangalia kwasababu kuna wakati unafikili jambo liko sawa ni mpaka wakati mgumu unapotokea ndipo unajijua kumbe mimi siko salama kama nilivyokuwa nafikili kwenye eneo la kifedha.

Eneo la pili ambalo linadhihilishwa ni thamani yako, kuna watu kutokana na changamoto zilizotokea sasahivi thamani yao imeshuka sana kwasabau kuna baadhi ya watu katika soko ujuzi wao hauhitajiki tena isitoshe wao wenyewe thamani yao imepotea kabisa

hakuna mahali wanaalikwa,kuuza, kununua, mtu anakuwa (reduced to zero) kwahiyo inadhihilisha kuwa kumbe hakuwa na thamani kubwa kama vile ambavyo alikuwa anafikilia na asipokuwa muangalifu pengine huko mbeleni anaweza akapoteza kila kitu ambacho alikuwa  nacho pia.

Eneo la tatu ambalo linadhihilishwa ni ukomo wa ujuzi wako (Limitation of skills) kuna wakati unajiona kama vile ni mtu mwenye ujuzi unaohitajika sana kwenye jamii lakini baadaye inapotokea hali ngumu kama hii ndipo unagundua kumbe ujizi wako siyo bora kama nilivyokuwa nafikilia.

Hii utaiona hasa wakati huu ujuzi wako hauwezi kukusaidia kuingiza pesa,kutatua matatizo yako, kupenya tafsiri yake ni kwamba pengine haukuwa imara kama ulivyokuwa unajiona. Kwahiyo kiufupi chakwanza kabisa hali ngumu kama hii inapotokea inakuja kudhhilisha maeneo gani tuko dhaifu.

Kwahiyo badala ya kulalamika na kunungunika unachotakiwa kufanya ni kujiuliza hivi jambo hili lililotokea ni maeneo gani yamenidhihilisha kwamba mimi niko dhaifu ili sasa ujipange.

Kusudi la pili wakati huu wa hali ngumu huwa inaibua watu wapya, kwenye kila changamoto siku zote usije ukasahau kuna watu wapya wataibuka kwasababu changamoto inatabia ya
kurudisha baadhi ya watu chini na kuimbua watu wengine juu. Kwa baadaye kuna watu wapya watatokea, kuna vipaji vipya ambavyo hatuvijui vitaimbuka kwasababu changamoto inasababisha watu waje na ubunifu wa aina fulani.

Lakini kuna viongozi pengine wataibuka wapya katika eneo mbalimbali na ambao tulikuwa hata hatuwajui vile vile kuna biashara mpya zitaimbuka ambapo toka zamani hazikuwepo, kuna majina mapya tutaanza kuyasikia kwahiyo kiufupi ni kwamba hali ngumu inapotokea kama hii huwa inaibua watu wapya.

Kwahiyo kikubwa ni kwamba mstari ambao unachorwa kuna watu wanashuka chini taratibu na kuna baadhi wanapanda juu taratibu .
Kusudi la tatu katika kipindi hiki kigumu ni kuleta style mpya ya maisha, baada ya changamoto hii tuliyonayo ukweli ni kwamba aina ya maisha ya watu yaani (life style) huwezi kuwa sawa sawa kama ilivyokuwa zamani . 
style ya maisha yatabadilika katika maeneo mbalimbali madharani, Afya, matumizi ya technology, fedha, tabia za kifedha,namna ya watu wanavyouza na  kununua.
Nini unatakiwa ufanye wakati huu mgumu ambao umeathili pakubwa.

Hakuna changamoto kubwa inapotokea inakuwa na hasara peke yake ndani yake kunakuwa na kufaidika kwa namna moja au nyingine na wewe unatakiwa uwe sehemu ya watu ambao hawazulika sana na changamoto hii.

Kukataa kuwa na fikra za jumla, wakati wote kunapokuwa na ungumu wa maisha kikawaida uwezo wa watu kufikili huwa unashuka . Uwezo wa kufikili unapokuwa unashuka madhara yake ni kwamba watu hawatumii muda mrefu kuchakata taarifa chochote kinachokuja mbele yao kinakuwa halali yao.

Kwahiyo hawapati muda wa kutafakari, kufikilia na hali ya ubunifu inakuwa imeshuka sana na hii  inasababishwa na mambo mawili makubwa, jambo la kwanza ni kwa sababu ya hofu (fear) mara nyingi kunapokuwepo na hali ngumu ya maisha watu wengi sana wanakuwa wanasumbuka sana na hofu

Mara nyingi  hofu huwa inaathili uwezo wa ubongo kufikilia ,inaathili uwezo wa ubongo kuja na suluhisho, inaathili uwezo wa ubongo kuwa na  alternative za maisha na njia mbadara. Jambo la pili ni kwasababu ya taarifa zinazofanana, sasa hivi mambo yamekuwa kama yamesimama kwahiyo mtu akiamuka asubuhi anapata taarifa zilezile mpaka anakwenda kulala

Kwahiyo hii inachangia kwamba watu hawana vitu mbadara, hawana mawazo mbadara kwasababu marighafi ya mtu kufikili ni taarifa ambazo anazokuwa anazipata hivyo kama hapati taarifa mpya hauthili uwezo wa kufikili upya  pia  hofu ikizidi watu wengi unakuta hawawezi kusoma, hawezi kusikiza kitu cha kumjenga,hawezi kusikiliza kitu ambacho ni chanya.

Amua kuwa mtu wa tofauti kwa maana kwamba usikubali kuwa na mawazo ya jumla . wewe lazima utafute taarifa nyingine kwasababu nyakati hizi kuna watu wanaendelea (gain), 

wanaendelea kutafuta njia mbadara kwasababu maisha kwa upande mwingine lazima yataendelea kwa namna moja au nyingine kwahiyo lazima uamue kuwa mtu wa tofauti uwe na mind ambayo iko taofauti na wengine.

Ukifikili kama mtu mwingine utapata matokea ambayo watu wengine wanapata pia.
Katika manunuzi nunua kile kitu ambacho unachokihitaji  siyo ambacho unakitaka ,kipindi hiki sicho cha kununua chochote kile unachokihitaji nunua kitu ambacho hasa unakihitaji siyo unachokitaka.

Huu siyo wakati wa kuspend wa kutumia ovyovyo kipindi hiki lazima uwe makini katika matumizi yako kabla hujatumia ni lazima ujiulize mara mbili mbili ni dhamu yako ya matumizi lazima iwe juu sana, nidhamu yako ya kifedha lazima iwe juu sana kabla hujafanya chochote inatakiwa ufikilie kwa kina kwa sababu hatujui changamoto hii itaendelea kwa muda gani na pia labda uwezo wako wa kujihudumia utadunu kwa muda gani

Fanya kitu cha mkakati , fanya kitu ambacho kitakusaidia kukupa matokeo kwa muda mrefu zaidi baada ya changamoto hii kwasababu kitu moja wapo unatakiwa ukijue ni kwamba changamoto inayotokea sasa hivi lakini madhara yake tunaweza kuishi nayo kwa muda mrefu sana na hapa kuna mambo matano unaweza kuyafanya moja unaweza kujenga ujuzi mpya,unaweza kupata ujuzi kwa wakati huu ambao unamuda mrefu ukiwa nyumbani umetulia .Tafuta ujuzi mpya unaweza kufanya katika njia ya mtandao

Jambo la pili unaweza kupata maarifa maalumu (specific Knowledge) maarifa fulani ambayo ni ya kipekee yanayoweza wewe kukusaidia kutoka sehemu moja mpaka nyingine madharani kusoma vitabu na kujifunza mambo mengine.

Jambo la tatu ni kuonesha uwezo wako kimkakati, kwa maana hiyo sasa ukifanya kitu cha tofauti ni rahisi sana kuonekana na kujulikana kuliko wengi ambao wanafikilia katika mtindo mmoja. Hivyo hakikisha unaimalika ule uwezo wako kimkakati katika maeneo ambayo unaweza kujiimalisha.

Jambo la nne unaweza ukatengeneza bidhaa au huduma mpya , kipindi hiki ni kizuri sana kwa kufanya hivyo kwasababu unapata muda wa kufikilia, kuchakata mambo, kuona zaidi ya kawaida, mara nyingi kitu inachoongeza ubunifu wa kitu ni ile hali ya kupata utulivu.

Changamoto hii itakapoisha kuna bidhaa nyingi mpya ambazo hazikuwepo duniani tutaanza kuziona kwasababu kila changamoto inatoa fursa na inaleta maisha ya tofauti ambayo pia mwanzoni hayakuwepo. Hivyo sasa ni wakati wako wewe kufikilia kitu ambacho kipya unaweza kukipeleka sokoni baada ya changamoto hii kupita bidhaa, au huduma kwa na namna wewe mwenyewe unaona.

Jambo la tano ni lazima upate muda wa kutafakari na kupanga upya maisha yako, jaribu kukaa chini pitia malengo yako, uwezo wako wa kifedha, nguvu ya ujuzi wako. Kwahiyo ni wakati ambapo unaweza kuangalia ni njia gani ambazo zinaweza kukuongezea kipato,nguvu ya kipaji chako na nguvu ya ujuzi wako.

Aina ya ujuzi au maarifa ambao unahitaji kuwa nao hasa kwa kipindi hiki kigumu
Uwezo wa kuchambu uwezo wako , katika hali hi kuna mambo mawili makubwa tunayoyaangali moja kuangalia ujuzi wako, kuna ujuzi ambao unaibuliwa pia mwingine hupotea . kwahiyo kaa chini jaribu kutafakari ujuzi ulionao sasa hivi baada ya changamoto hii kupita utahitajika zaidi au ndiyo utapotea au pengine utahitaji kuboresha zaidi ili ulete maana

Jambo la pili ambalo unatakiwa ni kuchambua uwezo wako wewe, ni uzoefu wako pengine umekuwa mzoefu kwenye jambo fulani ulikuwa ukijivunia huo uzoefu lakini je baada ya changamoto kupita uzoefu wako utakuwa na maana ?

Sasa unapofanya tathimini ya  uwezo wako,ujuzi,uzoefu wako kuna kitu kinaitwa (High Income Skills) au ujuzi ambao unaweza kukuongezea pesa kwa haraka na kwa kiwango cha juu.

Mabadiliko ya mfumo wa maisha ,uweze kujaribu kutathimini mfumo wa maisha kwa maana tabia ya maisha, kiafya ,kifedha,kijamii,kikazi kwa namna ya watu wanavyofanya mambo. Kila wakati changamoto inapotokea huwa inaleta fursa mpya, hali ya watu kupenda vitu vipya ambavyo zamani watu walikuwa hawavipendi, kudhamini vitu vipya ambavyo zamani vilikuwa havithaminiwi.

Na changamoto inapodumu kwa muda mrefu ule mfumo wa maisha unaanza kuwa ni sehemu ya kawaidi ya maisha ya watu katika eneo lile. Kwahiyo unatakiwa uwe na ujuzi wa kuchambua sasa madharani unachotakiwa kuangalia ni enao lako ambalo wewe unafanyia kazi au unapata kipato chako.

Kumbuka hutakiwi kufanya tathimini hii baada ya changamoto hii kuisha wale wanaofanya tathimini ya changamoto hii wanakuwa wameshachelewa sana wanaofanikiwa ni wale ambao wanafanya mapema kabisa kabla ya changamoto haijaisha ili uweze kujiaanda.

Technology preference sehemu hiyo siyo lazima sana uwe mtaalamu katika eneo hili, kunapokuwepo na changamoto ya maisha inasababisha technology ipate nguvu na nafasi madharani kwa sasa kuna baadhi ya shule ambazo zimelazimika  wanafunzi wake kusoma kupitia mitandao ya kijamii. Hivyo kwa sasa ni wakati ambapo unaweza kufikilia namna ambapo technology itakunufaisha ili uweze kuwafikia watu wengi.

Maarifa ya pesa, pesa huwa inabadilisha tabia yake kipindi kama hiki
Sehemu ambazo pesa hujificha wakati huu mgumu ambao ni changamoto kwa baadhi ya watu
Mawazo , kikawaida wanasema kwamba kila mwaka mwanadamu hupata mawazo takribani manne moja ya mawazo hayo akiamua kulifuatilia kwa umakini linaweza kumpatia kipato kizuri ambacho kinamuwezesha kuinuka kutoka sehemu moja mpaka kiwango kingine cha maisha yake.

Sasa wewe unatakiwa ujaribu kuwaza katika kitu ambacho unachokifanya kuna jambo gani ambalo unaliweza kulifanya likasaidia kupunguza au kuondoa hofu, ukiweza kupata jibu la swali hilo tafsiri yake ni kwamba watu watakuwa tayali kutumia pesa zao hata zile kidogo wanazo ili wapunguze kiwango kikubwa cha hofu ambacho wanacho. Kwahiyo sasa ni namna ya ewe kuja na wazo ambalo linaweza kuwaondolea hofu katika kipindi hiki.

Bidhaa, kuna bidhaa nyingi sana zinaendelea kutengenezwa katika kipindi kigumu kama hiki na nyingine zitaendelea kutengenezwa kwa sababu ya mabadiliko ya kimfumo na nyingine pia zitabunia kwasababu ya mabadiliko ya kimaisha. Hivyo sasa wewe ni kuangalia eneo la ujuzi wako ambayo wewe unaweza kujikita katika kuitengeneza, hapa siyo lazima utengeneze unaweza pia ukachukua sehemu ambazo zimetengenezwa ukawauzia wale ambao wanahitaji.

Ujuzi wako, kwa sasa hivi kuna aina nyingi ya ujuzi ambao utahitajika na siyo lazima mpaka ukasome shuleni mwingine unaweza kusoma kupitia kwenye mitandao ya kijamii lakini hakikisha baada ya changamoto hii kuisha unakuwa na ujuzi ambao utakupa kipato.

Matatizo, hapa kikubwa unachotaka kuangalia ni matatizo gani ambayo yameletwa na Corona sasa hapo utajianda kuchangua tatizo gani ambalo unahitaji kulitatua , kadri utakavyokuwa unatatua tatizo kubwa na ndogo ndipo utakapo kuwa unaongeza mwanya mkubwa wa kuwa na kipato kikubwa.

Sheria zinazoongoza matumizi ya pesa katika kipindi cha changamoto kama hichi
Sheria hizi zimetokana na wataalamu wawili ambao walifanya utafiti mkubwa sana mmoja anaitwa Gorger clasum ambaye  mwaka 1926 aliandika kitabu chake ambapo alieleza kanuni za dhahabu zinazohusiana na mambo ya fedha mwingine ni Mack
Phelps yeye mwaka 1977 alichapisha kitabu chake cha sheria za fedha.

Pesa ni matoke ya kufanya kitu ambacho watu wako tayali kukulipa kwasababu kinawapa faida fulani kwenye maisha yako, unapopata pesa tafsiri yake ni kwamba umefanya kitu ambacho watu wamekiona kimewapa faida kwenye maisha yao vile vile ukiona pesa imeacha kuja kwako hasa kipindi hiki cha changamoto ni kwasabau ya mambo mawili.

Jambo la kwanza ni huenda umeacha kufanya kitu kabisa hakuna kitu ambacho unakifanya kwahiyo matokeo yake ni kwamba hakuna mtu ambaye atakupatia pesa kwasababu hakuna kitu ambacho unakifanya

Jambo la pili nikwamba unafanya kitu lakini watu hawako tayali pengine kukulipa pesa madharani wanakiona hakina thamani au wanaona wanaweza kukifanyia wenyewe pia.
Hivyo pesa huja kwa mtu siyo jambo la ajabu tu au bahati nasibu ni matokeo ya kitu unachokifanya cha tofauti ambacho watu wanauhitaji nacho sana.

Fedha huongezeka kwa mtu ambaye anatafuta njia ya kutumia ili imletee faida zaidi na siyo suala la kuwa na pesa nyingi kikubwa ni namna mtu anatumia pesa yake . hivyo sasa fedha huendelea kumfuata mtu ambaye anaitumia kwa namna
ambayo inampa faida zaidi na kwa mtu ambaye anatapanya pesa fedha huwa na tabia ya kumkimbia
Sehemu kubwa na yamuhimu sana ni kuwa na budget na kujali pesa yako.

Pesa huenda  kwa wale wanaoamini kwamba pesa zipo kwa ajili yao , moja ya athali ya akili ya mtu ni kuamini kwamba kitu fulani hakiwezekani ukiamini kuwa hakiwezekani kiuhalisi hutokea . kwahiyo ondoa kitu kinachoitwa (Limiting belvies) hali yakutoamini katika mambo fulani kwa kufanya hivyo unafanya ubongo wako kutofikili mbele zaidi na ubongo ukiacha kufikili maana yake umeacha kupata fursa.

Hivyo sasa pesa huwafuata watu wanaoamini pamoja na changamoto zilizopo pamoja na magumu yalipo bado anafurusa ya kutengeneza na kupata pesa zaidi

Pesa huwa inamkimbia mtu ambaye anailazimisha kupata kipato ambacho hakiwezekani au anafuata ushauri wa walaghai au watu wajanja, katika kipindi hiki watu wengi wataanza kutapeliwa kwasababu kunawatu ambao wanataka kupata pesa kwa ghafla baada ya kuwa biashara zao zimeshuka au kipato

Hivyo sasa mtu ambaye anataka kupata pesa kwa haraka sana kwa namna isiyo ya kawaida ni kama vile wanajaribu kumlazimisha ng’ombe kumkamua atoe maziwa ambayo hana  matokeo yake ataishia kutoa damu.

Usiingize pesa yako katika mambo ambayo huyajui vizuri wala kuyafahamu kwasababu ya tamaa, njaa, shida,matatizo unaweza kujikuta hata kile kidogo ulichonacho unakipoteza pia
Fedha huwa inazidi kuongezeka na kumganda mtu ambaye anaiwekeza kama ambavyo anashauriwa na watu wenye hekima kwamba mtu wa aina hii akiwa amepata pesa yake hapeleki tu mahali popote.

Kwahiyo usichukue ushauri kwa mtu yeyote zigatia sana ushauri wa watu wanaojua kuhusiana na hilo.

Baada ya kujifunza mambo yote hayo jaribu kuyafanyia kazi kuna vitu vingi sana utapata, ushichelewe kufanya maamuzi kwasababu utapitwa na fursa nyingi, changamoto kadiri zinaendelea zinaleta dynamics kwa kubadilisha mambo fulani kwahiyo usiwe mgumu wa kujifunza kama kuna uwekezaji mkubwa ambao unaweza kuufanya kipindi hiki ni kujifunza

Madharani kupitia video,vitabu,redio,television,mitandao ya kijamii. Hii itakusaidia kubaki na ubora wako na kuzidi kufanikiwa wakati wote.