FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

RAY C AMPA MANENO YA BUSARA DIAMOND PLATNUMZ

Msanii mkongwe wa Bongo Fleva mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni, Rehema Chalamila  ‘Ray C’ ambaye pia ni dada wa wasanii wa muziki nchini, amemtaka msanii mwenzake Naseeb Abdul Diamond Platnumz ambaye pia ni mdogo wake kwenye sanaa kuishi kwenye maneno aliyowahi kuyazungumza.

Ray C kupitia ukurasa wake wa ‘Instar gram’ ali –‘share’ video hiyo  fupi ambayo alikuwa akizungumzia kuhusu ushikamo wa wasanii ili muziki ukue kimataifa zaidi.

“Hii ni kwako Diamond Platnumz Tusitengenezeane chuki neno kubwa sana dogo sana hebu ishi kwa hili neno ulilotamka hata Mungu atafurahi na atazidi kufungua baraka mbele yako acha maneno mengi wewe piga kazi tu uwanja wako mzee baba

Nakukubali sana sema kuna muda unakera dogo mimi ndiyo dada ako halafu nilishakwambia ukinimind kimpango wako ila nakukumbali sana na unajua sana sema una maneno fulani yani yanaudhi sana

siku niliyokutana na wewe tukaongea nilikukubali sana maana ulinioneshea upendo wa thati kutoka moyoni na kila mtu anayenijiua anajua kuwa nakukubali ila kuna watu fulani wanaokuzunguka wanakuharibia sana yaani vijembe hata havikupendezi mdogo wangu na hao wala hawakutakii mema wanakupamba tu ili mladi uharibu tu

hawana nia njema na wewe unapendwa sana sema mdomo dogo mdomo hebu tulia tupe tu minyimbo achana na hizi mambo aisee usitugawe mashabiki pleas!” alaindika Ray C. 
msanii mwenzake Rosa Ree alifunguka kwa kumwabia kuwa ushauri alitoa ni wakinafiki kwani umeegemea upande mmoja.

“Ushauri wa kinafiki tu kwa nini asitoe ushauri pande zote mbili??? Kwa nini tu Diamond ndo mwenye makosa??” Rosa Ree.
hata hivyo mashabi hawakusita kutoa ya moyoni baada ya ushauri huo

“Huyo dada hana akili huwezi kushauri sehemu moja tu saiv Diamond Platnumz wana mshambulia mbona upande wa pili ndo wameanzixha zari halafu anavunga anamkazia msanii wetu mwambie atuachie msanii wetu” aliandika mmoja wa mashabiki



                         ‘Asap Rocky’ anyimwa ruhusa hii
                                         

American rapper  Rakim Mayers ‘Asap Rocky’ amenyimwa ruhusa ya kutoa mavazi na kutumbuiza kwa wafungwa wa jela ambayo alifungwa nchini Sweden mwezi Julai mwaka huu.

Mwezi uliopita Rocky alisema ata-design mavazi kwa ajili ya wafungwa wa Jela hiyo. Kupitia ‘Twitter’ yake aliandika.

-"Even When I'm denied access to donate or perform for the inmates in Sweden I still want to raise awareness for the immigrants and poor people of outside surrounding areas, this has been a difficult journey, but I feel it's my task to give back to people who supported me when I was down." aliandika  Asap Rocky.   






“Nasikia baba Tiffah unasema eti Fiesta haikujaza” Nay wa Mitego
                                           


Msanii wa muziki wa kizazi kipya Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ ameutumia ukurasa wake wa ‘Instar gram’ kutupa dongo kwa Diamond kuhusiana na tamasha la Fiesta liliofanyika wikiendi hii katika uwanja wa uhuru jijini Dar Es Salaam.


ikumbukwe baada ya Tamasha la Wasafi Festival kumaliuzika tarehe 9 mwezi wa 11 na kufanikiwa kujaza uwanja kwa asilimia kubwa ambako lilifanyikia katika viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar Es Salaam
yalianza maneno ya kukejeliana kati ya pande mbili ambazo zimefanikiwa kufanya matamasha makubwa hapa nchini ambalo ni Tamasha la Wasafi Festival lililochini ya Wasafi Media na Tamsha la Fiesta lililochini ya Clouds media.

Maneno yalianza baada ya Tamasha hilo kujaza sana na watu kuanza kusema kuwa tutaona tamasha la Fiesta kama litajaza hivi lakini pia katikati kabla ya Tamasha la Fiesta kufanyika Dar Es Salaam yaliibuka maneno baada ya Diamond kwenda kufanya show nchini Siera lione na kufanikiwa kujaza uwanja watu walianza kumkejeli kuwa haikuwa show yake, na kupelekea Diamond kuandika maneno haya:-

Sasa baada ya Fiesta kufanyika wikiendi hii ambayo ilikuwa tarehe 8 mwezi wa 12 na kufanikiwa kujaza sana tena katika uwanja mkubwa kuliko uwanja lilikofanyika Tamasha la Wasafi Festival maneno yameanza mitandaoni tena hadi kupelekea msanii Nay Wa Mitego kutupa dongo kwa Diamond na kumwambia kuwa

“Nasikia BabaTiffa Unasema Eti Fiesta Haikujaa.? Nakujua Mwanangu Ukipanic Huwa Unakua Na Tatizo La Kuona, Sasa Relax Chukua Time Yako Tizama Hii Clip Kwa Dakika 1 Tu, Haija Editiwa ata Kidogo Utapa Jibu Na Utaendelea Na Kazi Zako Zingine. Pia Nikukumbushe Kitu, Mtoto Ni Mtoto Na Mama Ni Mama Tu.”alindika Ney
Hata hivyo baadhi ya mashabiki walipongeza Nay kwa kusema ivyo lakini wengine walmkosoa kwa kusema kuwa hakusitahili kusema hivyo kwani yeye mi msanii kuna leo na kesho

“Wewe mwenzio anatamasha lake lako liko wapi? ebu jifikilie nani mwenye tamasha apo kati yawasani wote apo utumwa mwanangu kila siku upo kwenu kwanza una kolabo gan namsani wanje uyo umuwezi kwa lolote mpaka kwa watoto mtumwa mkubwa jiongeze mambo ayo wachie wenyewe media zao” aliandika mmoja wa mashabiki.





      


           Uwoya sintovumilia hili kwa mume wangu
               
                     
Staa wa BongoMovie, Irene Uwoya, amesema atakuwa hana noma akimuona mpenzi wake anam 'kiss, mwanamke mwingine au kumuita majina ya kimahaba, ila kitu atakachokishindwa ni kuona mwenza wake akimsaliti.

Irene Uwoya,alisema  hayo baada ya watu kujaji urafiki wa Wema Sepetu na Aunty Ezekiel, kupeana mabusu hadharani jambo ambalo si la kawaida kwa wanawake kufanya hivyo.

"Mimi naona ni kawaida tu ni watu ambao wana urafiki wa muda mrefu, ku-kiss ni vitu vya kawaida tu hakuna kikubwa hapo haimanishi chochote hata kumwita mtu darling ni sawa tu, hata mimi mtu yeyote naweza kumuita hivyo" alisema Uwoya.

Aidha akizungumzia kuhusu mpenzi wake, kufanya kitendo cha kum 'kiss' mwanamke mwingine Irene Uwoya alisema.

"Kwangu mimi mwanaume wangu akimkiss mwanamke itategemea, unajua kuna kiss zinatofautiana ukifanya hivyo katika hali ya urafiki inaonekana na ukifanya katika hali ya mapenzi inaonekana pia, mimi nitachukulia kitu cha kawaida cha urafiki hakuna tatizo  ila akinisaliti siwezi kuvumilia" aliongeza .