FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

H BABA APANIA KURUDI KWA KISHINDO KWENYE ‘GAME’

Msanii wa Bongo Fleva, Hamis Baba ‘H Baba’ amesema mwaka 2020 ni mwaka wake kwani amepania kurudi kwa kishindo kwenye game.

H Baba alisema kuwa amekuwa mapumzikoni kwa muda wa miaka mitano sasa na ameamua kuyarejesha makali yake mapema mwakani ataachia kazi.

Katika kipindi cha ukimya wake kwenye ‘game’  kuna vitu vingi amejifunza ila anachukizwa sana na baadhi ya wasanii kuwa na tabia za uongo na kuifanya fani ya muziki kuwa kichaka cha maovu.

Aidha alifunguka kuwa wasanii wengi wamekuwa wakitunga nyimbo nyepesi sana tofauti nay eye.
Hivyo amejianda kikamilifu kabisa kuhakikisha muziki wake unarudi kwa kishindo zaidi ya hata ulivyokuwa  zamani.






Amber Rutty akataa kufananishwa na nabii Tito
 Msanii wa Bongo Fleva , Video vixen na mwanamitandao Amber Rutty, amekataa kufananishwa na nabii Tito kwa kusema hadhi yake ni ya kufananishwa na ‘role model’ wake ambaye ni mwanamitindo wa Marekani, Amber Rose.


Amber Rutty  ameeleza hayo baada ya kuwepo na ‘comments’ nyingi zinazosema kwamba sura yake na rangi yake, imefanana na nabii Tito.

“Kuna watu wanapenda kuongeaongea nifanane na nabii Tito kwani mume wangu au mpenzi wangu, sioni kama tumefanana hatuna hata undugu, nitafanana naye kivipi halafu yule ni mtoto wa kiume mimi ni wa kike wapi na wapi nifanane naye” alisema Amber Rutty.

Aidha Amber Rutty aliongeza kuwa “Tupo tofauti hatuwezi kufanana nataka nifanane na ‘role model’ wangu Amber Rose au mume wangu ambaye nipo naye kwa saa 24, na wala sijafanana na Amber Lulu hata kidogo mimi Rutty yeye ni Lulu” aliongeza.




Kamikaze agonga msumari wa mwisho kwa Vanessa Mdee 
Msanii wa Bongo Fleva  Cyrill Kamikaze amegongelea msumari wa mwisho kwa Vanessa Mdee na kusema, alivyomtolea lugha chafu hadhani kama alimaanisha ila alikuwa na hasira na mawazo na kwamba hawezi kumjibu chochote.

Kamikaze ameeleza hayo, baada ya kuulizwa kuwa  alichukuliaje kauli ya Vanessa Mdee, kumwambia hapendi wanaume ambao wana tabia za kike ambapo amejibu.

"Hilo lishapita labda tuweke msumari wa mwisho, sikuwahi kufanya chochote wala kuongea lolote kitu kilichotokea ni kati yake na Jux kwenye mapenzi yao, mimi sijawahi kuingilia na kujua chochote kama aliongea hivyo ni fresh"  alisema Cyrill Kamikaze.

Aidha aliongeza kuwa "Kwa yeye kuongea vile sijui alikuwa katika hali gani na alimaanisha nini, sijawahi kukaa naye kumuuliza lakini nina imani hakuongea kile kitu kwa kukimaanisha, unajua kuna muda unaweza ukaongea kitu kwa kuwa una hasira au mawazo kwa sababu ya vitu vingi, sijawahi kumhukumu na siwezi kurudisha neno lolote" aliongeza.






Chuchu Hansy akanusha kulindwa na silaha



Msanii wa Bongo Movies  Chuchu Hansy, amekanusha madai ya yeye kulindwa na silaha na mpenzi wake, ambaye pia ni mzazi mwenziye, Vincent Kigosi ‘Ray’

“Siwezi kulindwa kwa sababu mimi sijafikia hatua ya kulindwa na silaha, mtu akiamua kufanya jambo au kitu chake anafanya tu hata ulindwe kwa saa 24 atafanya tu ndani ya dakika hata 5 au sekunde". alisema  Chuchu Hansy

Aidha Chuchu Hansy ameongeza kuwa hawezi kumzungumzia baba watoto wake kuwa anafanya hivyo labda aulizwe mwenyewe.

"Siwezi kumuongelea kwa sababu ana vitu vyake, vingine ambavyo siwezi kuvizungumzia ni vizuri mkimuona mumuulize hilo swali, kama anayo au hana atawaonesha, sisi Watanzania hatuna desturi ya kulindana, hivyo nitaishi maisha ambayo Nchi yangu inaruhusu" aliongeza.





Juice Wrld avunja rekodi hii
 Baada kifo chake mwishoni mwa wiki , Rapa  Jarad Anthony Higgins ‘Juice Wrld’ kutoka Marekani, ashika rekodi ya kusikilizwa zaidi mtandaoni kwa muda mfupi.
Imeelezwa kuwa, kazi za rapa huyo zimesilikizwa mara nyingi zaidi mtandaoni.

Twakimu zinasema rapa huyo amesikilizwa mara milioni 38.2 (streamed 38.2 million times) baada ya kifo chake kilichotokea siku ya Jumapili.

Aidha, imeendelea kueleza kuwa, kusikilizwa kwa kazi zake kulipanda maradufu hadi kufikia 487% na kumfanya kuwa msanii aliyesikilizwa mara nyingi zaidi kwa muda mfupi.