FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

VODACOM YAUZA HISA ZA BILIONI 476/-



KAMPUNI ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania, imefi kia lengo la kuuza hisa zake 560,000,000 zenye thamani ya Sh bilioni 476 kama ilivyokuwa imepangwa.
Katika mauzo hayo yaliyoanza Machi 9, mwaka huu na kuhitimishwa Julai 28, mwaka huu ambapo kila hisa iliuzwa kwa Sh 850, mauzo ya asilimia 60 yamehusisha wawekezaji wa ndani wakati asilimia 40 imehusisha wawekezaji wa kigeni Kwa mujibu wa taarifa ya Vodacom kwa vyombo vya habari, taarifa ya mauzo ya hisa inazingatia idhini ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kuhusu toleo hili la Hisa, na kwamba wawekezaji ambao maombi yao yamekubaliwa wataingiziwa hisa zao katika akaunti zao zinazohifadhiwa na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Stakabadhi za Umiliki wa Hisa zinaweza kupatikana kutoka kwa mawakala ambako hisa husika zilinunuliwa. Toleo la Hisa za Vodacom Tanzania limekuwa toleo kubwa zaidi na la kihistoria kufanyika nchini, na kuhusisha Watanzania zaidi ya 40,000 wengi wao wakiwa wanashiriki kwa mara ya kwanza katika masoko ya mitaji hapa nchini.
“Kwa hiyo, Toleo hili limewezesha kupanuka kwa ushiriki wa wananchi katika soko la mitaji na dhamana, na pia katika uchumi wa Taifa,” ilisema sehemu taarifa hiyo. Hisa hizo zitaorodheshwa DSE na mauzo yake kuanza Agosti 15, mwaka huu. Kutokana na kukamilika kwa uuzaji huo wa hisa, Vodacom imeelezea kufurahishwa na kuwashukuru Watanzania kwa uamuzi wa kuiunga mkono kampuni hiyo.