FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

MAONESHO YA NANENANE YAANZIE NGAZI YA KATA


HALMASHAURI za Wilaya za Mikoa ya Kanda ya Mashariki inayoundwa na Tanga, Pwani, Dar es Salaam na Morogoro ambazo hushiriki maonesho ya kilimo, mifugo na uvuvi (Nanenane), zimeshauriwa kuanzisha ngazi ya kata na wilaya.
Hii ni kuiwezesha elimu inayotolewa na wataalamu kwa wakulima na wafugaji kuhusu teknolojia ya kilimo, ufugaji, mbegu bora na matumizi ya pembejeo za kisasa iwafikie wakulima wengi zaidi waliopo vijijini.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari alibanisha hayo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wataalamu wa sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kwenye Uwanja wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Katibu Tawala wa mkoa huyo pia alishauri mikoa ya kanda hiyo baada ya kumalizika kwa maonesho hayo ni vyema kufanyika katika onesho la Kilimo kwa kushindanishwa mkoa kwa mkoa ili kupata wakulima na wafugaji mahiri ambao wanaweza kuingia kushindana.