FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

Dkt.HUSSEIN MWINYI AHIMIZA UTENDAJI KAZI KATIKA UKUSANYAJI MAPATO

 



Na, Kalebo Mussa,Dar Es Salaam.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewataka viongozi na watendaji wa Wizara na idara za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutekeleza wajibu wao katika kusimamia mifumo ya ukusanyaji na matumizi ya fedha za Serikali.

Akizungumza Ikulu jana visiwani Zanzibar katika kikako cha kupokea ripoti ya mthibiti na mkaguzi mkuu wa serikali (CAG) Dkt. Othamani Abass Ali, alisema kuwa hategemei ripoti ijayo ya mwezi June, 2022 kuwepo lundo la dosari.

Alisema lazima hali hii ilekebishwe mara moja kila mtu atimize wajibu wake kwani taasisi nyingi za serikali hazijatimiza wajibu wake ipasavyo katika ukusanyaji wa mapato.

 “Baada ya kupokea ripoti hii nadhani kila mmoja wetu aone wajibu wake katika kurekebisha hali, leo ni sisi tunaozungumza fedha za OS hazitoshi, fedha za miradi ya maendeleo hazipatikani”, alisema Mwinyi.

Dkt. Mwinyi alisema ripoti hii inaonesha  kuna sehemu nyingi tungetakiwa tupate fedha kama serikali lakini hazipatikani kutokana na kutokuwa makini katika kukusanya mapato.

Aidha, Dkt. Mwinyi aliwakumbusha mawaziri kutembelea katika taasisi zao ili wazijue vizuri ili kuhakikisha taasisi hizo zinafanya wajibu wake ikiwemo ukusanyaji wa mapato ya serikali ili kuondoa dosari ambazo zinajitokeza.

Awali, mdhibiti na mkaguzi mkuu wa serikali (CAGD) Dkt. Othamn Abass Ali alisema  katika kukamilisha ripoti hiyo kuna taarifa ambazo waliziomba wakazikosa.

Alisema  wakati wa ukaguzi alibaini agizo la kuhamisha fedha ya mapato yanayotokana na kodi ikiwemo mapato ya ZDRB yaliyokusanywa kupitia hesabu yake iliyopo PPZ kwenda BOT mpaka kukamilisha ukaguzi huo, ukaguzi haukupatiwa agizo hilo.

“Mapato ya TRA yalikuwa yakihaulishwa kutoka hesabu yake iliyopo PPZ kwenda BOT mara tatu kwa wiki, lakini huku kwetu sisi ZDRB, PPZ, BOT hatukupata haya maagizo na kilichobaini ni kuwa hii fedha ina kaa sana pale, hali hii ni kuikosesha serikali kufanya matumizi ya fedha hiyo kwa wakati”, alisema Ali.

Hata hivyo, alisema  katika ukakuzi huo ulibaini kuwa taasisi ya utafiti wa kilimo Zanzabari haina mfumo mzuri wa utayarishwaji wa bajeti katika vyazo vyake vya mapato.

 Alisema hali hiyo imetokana na kuwepo na mabadiliko ya mwaka ya makadirio ya mapato yanayotokana na uuzwaji wa miche, mazao, pamoja na mapato ya ukondishwaji mashaba ambayo hupanda na kushuka bila kuwepo na sababu za msingi.