FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM
Showing posts with label afya na mazingira. Show all posts
Showing posts with label afya na mazingira. Show all posts

FAHAMU UGONJWA WA KIUNGULIA NA MATIBABU YAKE

 

 

Na Mwandishi Wetu.

Kiungulia (kwa Kiingereza heartburn) ni hali ya kusikia maumivu makali katika koo la chakula.

Maumivu hayo yanatokana na kupanda kwa asidi iliyomo tumboni (asidi haidrokloriki = HCl) inayofanya kazi ya kuua vijidudu vinavyoingia tumboni kwa njia ya chakula na maji. Mara nyingi kiungulia hutokea baada ya tumbo kujaa gesi

Kiungulia kinaweza kuwa na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kula kwa pupa au kupita kiasi, matumizi ya dawa za kulevya, ujauzito, tumbo kujaa gesi, vidonda vya tumbo.

 

Namna ya kuzuia kiungulia

Kiungulia kinaweza kuzuiwa kwa namna mbalimbali. Zifuatazo ni baadhi ya njia za kuzuia kiungulia:

Epuka kulala mara tu badaa ya kula chakula.

Epuka kula kupita kiasi.

Epuka kula vitu kama maharagwe, mboga za sukuma n.k.

Epuka vinywaji vyenye asidi kwa wingi, mfano: soda n.k.

EEpuka matumizi ya dawa za kulevya.

 

Matibabu ya asili ya kiungulia

 

1.Apple cider vinegar

Apple cider vinegar au siki ya matunda ya apple inasaidia kurekebisha utindikali kwenye tumbo na hivo kupunguza acid ya tumboni. Nenda supermaket au sokoni tafuta apple vinagar yenye sifa hizi

 Organic

 Unfiltered

 With the mother

 

2.Baking soda

 Baking soda ni moja ya bidhaa ingine inayopatikana kwa urahisi itakayokutibu kiungulia chako. Kumbuka tu kwamba kuna tofauti kati ya baking soda na baking powder. Ukienda dukani au supermaket ulizia baking soda.

3.Juisi ya Aloe vera

Aloe vera ni moja ya mimea adhimu sana kutokea kwani inatibu magonjwa mengi. Hakikisha unapata juisi salama ambayo haijawekwa kemikali mbaya. Mmea wa aloe vera ni mchungu sana, kabla hujaanza kutumia tafuta kwanza kwenye maduka ya tiba asili kama utapata juisi ya aloe vera iliyopunguzwa makali.

 

Matumizi ya aloe vera kutibu kiungulia

 Kutibu kiungulia kunywa robo kikombe cha juisi ya aloe vera kila siku asubuhi kabla hujala chochote. Endapo utakosa juisi, unaweza pia kutafuta vidonge vya aloe vera vitakufaa sana kutibu kiungulia.

 

4.Tangawizi

 Tangawizi moja ya dawa asili kabisa ya kutibu maumivu ya mwili. Pia tangawizi ni nzuri kwa kuuimarisha usagaji wa chakula tumboni na kuzuia asidi ya tumbo kupanda juu. Tangawizi pia inazuia athari ya bakteria wabaa tumboni.

 

Matumizi ya tangawizi kwa kiungulia

 Kutibu kiungulia, tengeneza chai ta tangawizi na unywe baada tu ya kumaliza kula.

 

5.Binzari nyembamba(Cumin)

 Moja ya tiba ingine makini sana ya kiungulia inayopatikana jikoni kwako ni binzari nyembamba ambayo hutumika sana kwenye kupika pilau. Gesi inapojaa tumboni inaweza kusababisha kiungulia pia. Kutumia binzari nyembamba itakusaidia kuondoa gesi tumboni a hivo kuepusha kiungulia.

Matumizi ya binzari nyembamba

 Chukua kijiko kimoja cha bidhaa nyembamba chemsha pamoja na maji nusu lita kisha kunywa mara tatu kwa siku baada ya mlo wako.

 

6.Tui la nazi

Utashangaa kwamba kiungo hichi ambacho umekuwa ukitumia kila siku kupika wali na maharage, kinaweza kutibu changamoto yako ya kiungulia pasipo kumeza dawa.

Matumizi

 

Baada ya kukuna nazi yako, weka machicha ya nazi kwenye sufuria, sagia na tangawizi kidogo pamoja na maji lita moja kisha chemsha kwa dakika 5 epua. Chuja tui lako kisha kunywa glass moja asubuhi na jioni kabla ya kula.

NB: Kumbuka wataalamu wa Afya wanashauri kwamba wakati wa kulala ni vyema utumie mto.

 

FAHAMU MUAMKO WA VIJANA KUPIMA VIRUSI VYA UKIMWI

 

 


Na Mwandishi wetu.

MUAMKO wa vijana kwenda kupima Virusi vya Ukimwi na kupata ushauri nasaha umekuwa mdogo sana kwani ni idadi chache ya vijana wanaoenda kupata huduma hiyo.

Akizungumza na Nipashe Mshauri kutoka Zahanati ya Kinyerezi Jijini Dar Es salaam, William Michael alisema kuwa watu wengi wanaogopa kwa sababuu ya ugojwa wenyewe jinsi ulivyo.

“Wanaokuja kupima wenyewe kutoka nyumbani ni wachache sana ukilinganisha na wanaopima kutokana na dalili ambazo anaonesha mgonjwa, ambapo wanaokuja wenyewe kwa Julai 1 mpaka 30 mwaka huuwalikuwa 42 na 209 wakiwa ambao wanapimwa kutoka na dalili walizonazo,” alisema Michael.

Alisema vijana wanakitu kinachoitwa hofu ya utambuzi kwamba hufikilia endapo atakutwa na maambukizi itakuwaje, hofu hiyo imekuwa kubwa kwasabau ya aina ya ugonjwa kuwa mkubwa.

Aliendelea kusema kuwa mtindo wa maisha hususani wanaume hujikita katika shughuli za utafutaji ukilinganisha na wanawake hivyo kushindwa kufika katika vituo husika, vilevile wanaume wengi huwa na tabia ya kupuuza masuala ya kucheki Afya zao.

“Wanaokuja kupima sana ni wanawake ukilinganisha na wanaume, ukiona mwanaume amekuja kupima inabidi umpe kipaumbele na atakupa mambo mengi kulingana na vitu vingi alivyopitia,”alisema Michael.

Aidha, Michael alisema kuwa ili uweze kukaa vizuri kama kijana hutakiwi kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na mtu ambaye hujui hali yake ya kiafya, kabla haujingia katika mahusinao hakikisha unajua hali ya kiafya ya mwezio pia historia yake.

Kuwa na mtu mmoja katika mahusiano ambaye mnaaminiana, vilivile vijana watumie kinga ili kulinda afya zao dhidi ya maambukizi ya Ukimwi.

 Ahamedi Saidi ambaye ni mmoja yawaliofika kituoni hapo kupata ushauri nasaha alisema kuwa yeye kila mwezi huwa anautaratibi wa kwenda kucheki afya ili kujua maendeleo ya afya yake.

“Nakumbuka kipindi nasoma walimu walikuwa wanatufundisha kuwa kucheki afya katika mwili wa binadamu ni muhimu sana ili kujua uko katika hali gani, kadri nilivyokuwa naelewa kila mwisho wa mwezi kwa sasa ni lazima nicheki afya,” alisema Saidi.

Pia aliwashauri vijana wajitokeze kwa wingi kwenda kucheki afya zao ili wajue afya zao kama wanamaaumbukizi ya Ukimwi ni muhimu sana kwa vijana kucheki afya.

 

 

 

 

 







Kategori

Kategori