FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

ZUCHU AVUNJA UKIMYA KUHUSU DIAMOND PLATNUMZ

 

                          Msanii wa Bongo Fleva Zuchu kutoka katika lebo ya Wasafi WCB.



Na Kalebo Mussa.


Msanii wa Bongo Fleva kutoka katika lebo ya Wasafi WCB  Zuhura  Othumani 'Zuchu' amevunja uvumi wa kutoka kimapenz na bosi wake Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz. 

 Akizungumza leo katika mahojiano na Wasafi Fm alisema kuwa yeye na bosi wake  Diamond Platnumz hawapo katika mahusiano ya kimapenzi kama watu wanavyotofsiri.

 Alisema huenda maneno au uvumi huo unatoka na ukaribu alionao wa kikazi na bosi wake, kwani mara nyingi amekuwa karibu naye kwaajili ya kumpa maelekezo ya kazi yake ya mziki.

 "Mimi na Bosi wangu hatopo kwenye mahusiano kama watu wanavyotofsiri yeye ni bosi ataendelea kuwa bosi" alisema Zuchu.

 Uvumi huu umekuja mara baada ya taarifa kusambaa mitandaoni kuwa wawili hao wanamahusiano ya kimapenzi na wameshavalishana Pete ya uchumba.