FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

TETESI ZA SOKA ULAYA AUGUST 25,2024


Juventus wameomba Manchester United kulipa sehemu ya mshahara wa Jadon Sancho ili kusaidia kuwezesha uhamisho wa winga huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 24. (Gazzetta dello Sport - in Italian)

Arsenal watamlenga mshambuliaji mwingine watakapokamilisha dili la kumsaini kiungo wa kati wa Uhispania Mikel Merino, 28, kutoka Real Sociedad. (Mirror)



Wolves wako kwenye mazungumzo ya kumsajili winga wa timu ya Burnley mwenye umri wa miaka 19 na Luca Koleosho wa timu ya taifa ya Italia ya Chini ya miaka 21. (Express & Star)

Leicester City wako kwenye mazungumzo ya kumsajili kiungo wa kati wa Morocco Bilal El Khannouss, huku Genk ikitaka angalau pauni milioni 17 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20. (HITC)

Kiungo wa kati wa Chelsea Tino Anjorin, 22, amekubali kwa mdomo kujiunga na Empoli inayoshiriki Ligi ya Serie A, huku mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Uingereza akihama kwa uhamisho wa bila malipo. (Fabrizio Romano)

Kipa wa Brazil Alisson, 31, yuko tayari kusaini mkataba mpya na Liverpool baada ya kukataa ofa kutoka Saudi Arabia, lakini Reds wamemtambua mrithi wake wa muda mrefu, mlinda lango wa Georgia Giorgi Mamadashvili, 23. (Telegraph - subscription required)

Mshambuliaji wa Brazil Vinicius Jr, 24, atasubiri hadi mwisho wa msimu huu kabla ya kufanya uamuzi wa kuhamia Saudi Arabia. (ESPN)

Real Sociedad wako kwenye mazungumzo ya mwisho mwisho ya kumsajili beki wa zamani wa Ujerumani Mats Hummels, 35, ambaye yuko kama mchezaji huru baada ya kuondoka Borussia Dortmund mwishoni mwa msimu uliopita. (Athletic - subscription required)

Mshambulizi wa Everton Neal Maupay, 28, anafuatilia kwa karibu kurejea nchini kwao Ufaransa na klabu ya Nice ya Ligue 1. (Nice-Matin - in French)