FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

BARCELONA WAMETHIBITISHA KUMSAJILI AUBAMEYANG

 

  Mchezaji  ambaye amesaini mkataba Bercelona akitoka Arsenal,  Pierre Emarick Aubameyang.


Barcelona na Pierre-Emerick Aubameyang wamefikia makubaliano ya mchezaji huyo kujiunga na Klabu hiyo baada ya mshambuliaji huyo kusitisha mkataba wake na Arsenal.

Jinamizi la Pierre-Emerick Aubameyang Arsenal limekamilika, huku mshambuliaji huyo akijiunga na miamba ya Uhispania Barcelona kwa uhamisho wa bure na kusaini mkataba wa miezi 18.

Barcelona wamethibitisha dili hilo Jumatano kwa video iliyoandikwa kuwa 'Ni Wakati wa Auba'. Walitangaza mkataba huo nje ya dirisha la uhamisho barani Ulaya kufungwa kwa sababu Aubameyang aliwekwa kama mchezaji huru baada ya mkataba wake na Arsenal kukatizwa.

Aubameyang alivuliwa unahodha wa Arsenal mwezi Desemba na meneja Mikel Arteta, akaamriwa kufanya mazoezi peke yake na kuondoka nje ya kambi yao huko Dubai na kuchelewa kurudi kutoka kwa safari iliyoidhinishwa na klabu kwenda Ufaransa.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 alipigwa picha akiwa Barcelona siku ya Jumatatu - kwa mshangao wa Arsenal na timu ya Uhispania - lakini ilimwacha katika nafasi nzuri ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu na kukamilisha uhamisho wake.

Alikuwa na mwaka mwingine kwenye mkataba wake wa Arsenal, ambao ulikuwa na thamani ya £350,000 kwa wiki na amepunguza masharti hayo kujiunga na Barcelona.

Huko Uhispania, Aubameyang ataongoza kikosi cha Xavi kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa msimu ujao.

Baada ya mwanzo mbaya wa msimu, Barcelona wako pointi moja nje ya nne bora na watacheza na Atletico Madrid walio nafasi ya nne Jumapili katika mchuano mkali.

Kwa sasa, haijulikani ikiwa Aubameyang atakuwa fiti vya kutosha kucheza mechi yake ya kwanza wikendi hii. Ingawa amekuwa akifanya mazoezi peke yake wakati wa uhamisho wake wa Arsenal, hajacheza kwa ushindani tangu alipocheza akitokea benchi dakika ya 85 katika kipigo cha 2-1 kutoka kwa Everton mnamo Desemba 6.

Katika hatua moja siku ya Jumatatu, dili hilo lilikatizwa na Arsenal walikuwa wakijiandaa kwa matarajio ya kurekebisha mambo na kumuunganisha tena Aubameyang.

Mkataba huo ulionekana kuporomoka kutokana na pande hizo mbili kushindwa kufikia mwafaka kuhusu jinsi ya kugawanya mishahara ya Aubameyang, huku Barcelona wakihangaika kutoa kiasi ambacho kiliiridhisha Arsenal na pia kukidhi vikwazo vyao vya kifedha.

Hata hivyo, mazungumzo hatimaye yalifufuliwa na kufungwa kwa misingi ya kawaida.

ubameyang alikuwa Arsenal kwa miaka minne  licha ya kuondoka katika hali mbaya, alifunga mabao 92 katika michezo 163 aliyoichezea klabu hiyo.

Kumruhusu Aubameyang kuondoka bila kusajili mbadala wake kunawakilisha kamari kubwa kwa Arteta na Arsenal na kuwaacha chini washambuliaji wawili pekee - Alexandre Lacazette na Eddie Nketiah - ambao wote mkataba wao unamalizika mwishoni mwa msimu.