FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

MAKAMBA AKANUSHA TAARIFA YA UHABA WA MAFUTA

 



Na, Kalebo Mussa, Dar Es salaam.

WAZIRI wa nishati, January Makaba amekanusha taarifa ya uhaba wa mafuta kwa siku 15 kama ilivyotolewa na mkurugenzi wa TPDC, Dkt. James Mataragio.

Makamba ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo alisema hakuna uhaba wa mafuta, hakuna haja ya watu kuwa na taharuki.

“Takwimu za mafuta ya taa nilizonazo ni za siku tano zilizopita, ambapo nchini kulikuwa na lita 3,978,276 zinazotosheleza kwa mahitaji ya siku 46” alisema Makamba.

Akijibu swali la mdau alieuliza mkanganyiko kati ya mkurugenzi wa TPDC na kauli yake kujichanganya, Makamba alisema kauli yake ni ya uhakika ya Serikali.

 “Hakuna uhaba wa mafuta nchini. Hakuna sababu ya kuwa na taharuki. Utaratibu wa kuingiza mafuta unahakikisha kwamba mahitaji yapo wakati wote. Serikali inaendelea kuchukua hatua kuongeza uhakika wa upatikanaji na unafuu wa bei”, alisema Makamba.

Aidha , amemtaka mkurugenzi wa TPDC aende ofisini kutoa maelezo kabla hajachukuliwa hatua za Zaidi.