FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

SIRI YA UFANISI WA NANDY KIMUZIKI


Mwanamuziki wa Bongo Fleva Nandy , ameeleza siri ya ufanisi wake katika kazi ya kimuziki, ni kufanya kitu kwa kujitoa na kuelekeza nguvu zote na kuhakikisha lengo linatimia.

Nandy anaamini kuwa kufanya muziki mzuri ambao unavutia kwa namna moja au nyingine pia wenye maudhui mazuri ni moja ya kufika mbali kimuziki

“kikubwa ni kufanya muziki mzuri unajua wananchi nao saiviwanaelewa muziki kwahiyo ukifanya kitu kizuri au kibaya lazima watakwambia kitu ambacho napenda sababu ni moja ya kujifunza zaidi kwangu” alisema Nandy.

Aidha aliwataka mashabiki wake katika mwaka huu kutalajia kupata mziki mzuri pia na kufanya korambo na wasanii wan je lengo ikiwa nikupanua mbawa za kimuziki kuelekea kimataifa zaidi

Najua watu wengi walikuwa wanatamni na kuona nafanya kolabo na watu wa nje, niwahakikishie mwaka huu nimeamua kujipanga kikamilifu kuanzia video, niko siliasi na muziki sababu nimeona unalipa sana hivyo washabiki wangu wategemee muziki muzuri” aliongeza

Hata hivyo msanii huyo anampango wa kuanzisha biashara ambayo ni moja ya ndoto katika maisha yake kuachilia mbali na muziki ambao anafanya.

“Nampango wa kuanzisha biashara nyingi nitafungua kampuni mbili tatu za kibiashara nitaajiri watu wengi ili kuhakikisha tunafika mbali kimaendeleo” alisema Nandy

Nandy aliwahi kuwa na skendo za video zake ambazo hazikuwa na maadili kusambaa mtandaoni kitende ambacho siyo heshima kama msanii ambaye ni kioo cha jamii