FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

WAYNE ROONEY ATOBOA SIRI KUHUSU MANCHESTER UNITED

 

                                Wayne Rooney.


Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Wayne Rooney amekiri kuwa na kiburi mara baada ya  Sir Alex Ferguson alipojaribu kumsajili, meneja huyo wa Derby County alifichua kuwa Red Devils walijaribu kumsajili alipokuwa na umri wa miaka 14 pekee.

Rooney  alikataa ofa hiyo ili abaki na timu yake ya utotoni Everton, alisema Sir Alex Ferguson alijaribu kumsajili alipokuwa na umri wa miaka 14. Alex aliongea na wazazi wake Rooney kwenye simu na kumpa taarifa ya kuwa mwanao kuhitajika Manchester lakini Rooney hakuwa tayari kwa muda huo.

Kauli ya Rooney alisema kwamba yeye anahitaji kubaki Everton. Alex alizungumza kwenye simu  na mama na baba yangu. Alex alisema,  Manchester United wanataka kukusajili.’ Nikasema, ‘Mwambie aondoke. Nataka kuichezea Everton,

Kisha, kadiri muda ulivyosonga, nilijua kwamba nilipaswa kumchezea Alex Ferguson, sababu ya mimi kusajiliwa na United ilikuwa Alex Ferguson.” Alisema Rooney.

 Wayne Rooney bila shaka alikuwa mmoja wa vijana waliokuwa wakitafutwa sana katika soka la Uingereza wakati huo. Fowadi huyo wa Uingereza alicheza mechi yake ya kwanza Everton akiwa na umri wa miaka 16 na aliichezea misimu miwili kamili. Baadaye akahamia Manchester United katika msimu wa joto wa 2004 kwa ada ya karibu pauni milioni 26.