FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

HUMPHREY POLEPOLE AMKINGIA KIFUA TID


Katibu wa Itikadi na Uenezi (CCM), Humphrey Polepole amemkingia kifua msanii wa Bongo Fleva, Khalid Salum Mohamed ‘TID’ mara baada ya

kutumia msemo wake wa ‘Ni Yeye’ na chama pinzani bila ruksa kutoka kwake.

Humphery amesema kuwa kwa kitendo kilichofanywa kwa msanii huyo siyo haki kabisa kwani walipaswa kukubaliana kabla ya kutumia msemo huo.  

“Nampa pole TID sababu hawa majamaa ni mazulumati wametudhulumu wimbo wa Taifa. TID anapambana mtu wa watu ametengeneza Ni Yeye na ile ilikuwa Magufuli, wale majamaa wameichomeka kule. Hawajamshirikisha hawajamuomba kwa kweli sisi kama Watanzania tutawachukulia hatua” Humphrey Polepole alisema.

Aidha Polepole ameshangazwa na waliobadilisha wimbo wa Taifa kwa kuogeza ubeti watatu kwa manufaa yao bila kujua kuwa ni kinyume na sheria

“Nchi hii inatambulishwa ulimwenguni kwa vitu vikubwa vitatu, Moja kwa jina lake ambayo inaitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pili ni Bendera yetu, na kitu cha tatu kinachotutambulisha ni Wimbo wetu wa Taifa bila ya kujali tofauti zetu hapo juzi wenzetu wamebadilisha maneno ya wimbo wa taifa wameweka ya chama chao, najiuliza mbona sisi CCM tuna nyimbo nyingi nzuri lakini tunaheshimu huu mmoja hatuwezi kuunajisi kwa kuweka maneno binafsi."  Polepole alisema.


MADEE ATOA WAZO KWA WASANII WENZAKE


Mara baada ya msanii wa Bongo Fleva, Herry Samir ‘Mr Blue’ kuanguka jukwaani wakati anatumbuiza katika tamasha la nyama Choma, Madee ameibuka na wazo la kuwataka wasanii kukata bima za maisha.

Madee kupitia ukurasa wake wake wa Twitter aliandika ujumbe huo ambapo alimpa pole msanii huyo na kisha kutoa wazo la kukata bima za maisha na siyo kuishia kuwa na bima za magari kwa kuogopa matraffic

"Nimeona video Herry Samir Mr blue ameanguka jukwaani, natoa pole kwa niaba ya wanamuziki wote, Mungu akusimamie urudi tena kazini

"Ifike muda sasa wasanii mjikatie bima za maisha yenu, msikimbilie kukata bima za magari kisa unaogopa kukamatwa na traffic, hizi ajali za majukwaani zimekua nyingi siku hizi, hela uliolipwa unaenda kujitibia ni wazo tu" aliandika Madee Madee.

Suala la kuanguka kwa wasanii wakati wakitumbuiza katika majukwaa limekuwa likitokea sana madhara H. Baba, Gig Money ni moja ya wahanga na wengine.


Hata hivyo rapa huyo mpaka sasa anaendelea vizuri toka apate ajali hiyo Mungu aendelee kumlinda dhidi ya mjanga hayo.



MENINAH ACHAFUA HALI YA HEWA


Mashabiki wamechukizwa na tabia ya muigizaji wa filamu Bongo, Meninah Attick baada ya kuposti video kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa anafanyiwa masaji na mwanaume.