FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

ZUCHU AINGIA KWA KISHINDO WCB, AWEKA NIA HII

Habari kubwa ya kiburudani katika mtandao wa kijamii ni kuhusu lebo kubwa ya burudani nchini Wasafi (WCB) ambayo iko chini ya C.E.O. Naseeb Abdul  kumsaini msanii mpya wa Bongo Fleva wa kike, Zuchu ambaye mpaka sasa anatamba na wimbo wake uitwao ‘wana’.
Zuchu ameonesha kufurahishwa sana kwa kuingia mkataba na lebo hiyo ambayo inaaminika pakubwa kuwa inaubunifu mkubwa katika burudani kitaifa na kimataifa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram wa msanii huyo amefunguka maneno ambayo dhahili ni furaha kubwa kwake kwa kuwa sehemu ambayo itampa nguvu za kupanua mbawa zake zaidi ili kufikia malengo yake zaidi.

 “It's a huge honor to finally fulfill my dream, na pia ni baraka na bahati kubwa sana to be signed under The biggest label in Africa Wcb Wasafi
“Nikiwa kama mwanamke ndoto yangu kubwa ni kutumia kipaji changu kuthibitisha ule usemi "Power's not given to you. you have to take it" yaani "nguvu haiji kwa kupewa, bali kwa kujitengenezea mwenyewe".

“Na hii ni ili kufuta imani na dhana potofu kuwa wanawake hawawezi bila ya kuwezeshwa.
“Na muhimu zaidi pia safari yangu katika muziki iende kuwatia nguvu wanawake wote kupambana katika kutimiza ndoto zao.
Kwa zaidi ya miaka minne niliisubiri siku hii.
“Thank you  Diamond Platnumz and whole of Wcb Wasafi Management for believing in my talent expect the absolute best.
To all music lovers from all Over the world, ninaitegemea sana support yenu.

“Asante Mwenyezi Mungu kwa kipaji na nafasi hii, Ninakuomba uniongoze katika njia yenye Mafanikio”. aliandika Zuchu
Achilia mbali na hilo Diamond Platnumz kupitia ukurasa wake wa Instagram hakusita kutoa neno ambapo alimtaka msanii huo kuwa kielelezo kwa wanaweke wengine kujiona kuwa wanaweza ambapo wanapofanya juhudi ya kutimiza ndoto zao.

“kupitia wewe na sapoti ya wadau na mashabiki, tukabadilishe mtazamo na fikra potofu na ulimwengu wajue kuwa mwanamke ukimuwezesha anaweza” aliandika Diamond Platnumz.
Hata hivyo msanii mwenzake wa kike Faustina Charles Mfinanga maarufa kama Nandy alifunguka ya moyoni kwa kuona kuwa tasnia ya burudani sasa inaenda mbele zaidi kwa kuwa na ongezeo la wasanii wa kike.

“Hongera sana Zuchu am proud of you! another queen in Tanzania tusogeze  Bongo Fleva mbali zaidi nakuamini” aliandika Nandy
Vilvile nao mashabiki hawakuwa nyumba kutoa maoni yao juu ya suala hili ambalo wengi wao wameoneshwa kufurahishwa na kusainiwa kwa msanii mpya katika lable hiyo.
Mapokeo yao yamekuwa makubwa hasa kupenda wimbo wake mpya ambao unafanya vizuri sasa.
Kwa maana hiyo sasa Zuchu atakuwa imetimiza idadi ya wasanii sita, Naseeb Abdul, Mbosso, Lava Lava,Rayvvan, Quuen Darlin, Zuchu.

Zuchu ni mtoto wa malkia wa taarab nchini Tanzania, Khadija Omary Kopa, mama huyo alimpa maneno ya busara mwanae ambayo hakika ni furaha kubwa
“Kila hatu Dua, Allah akuongoze Mwanangu imekuwa ndoto zako kwa miaka mingi sana na leo umetimiza nusu ya ndoto hizo kilichobaki ni dua na salaa nyingi ili Allah azid kukusimami, Nimefurahi Sana Sana na Allah awasimamie nyote wewe na Ma boss zako na wenzio wote unaofanya nao kazi mzidi kuendelea kufanya mazuri na makubwa, Tulia upo sehemu salama mama, Nakupenda Sana Mwanangu” aliandika Khadija Koppa katika ukurasa wake wa Instagram.

Khadija Koppa alifunguka namna mwanaye alivyokuwa na furaha kubwa ya kuwa sehemu ya Wasafi
“Yani sijalala kwa amani kwa furaha maana kama siamini,tumemfuta sana machozi mpaka leo kafikia hapa Basi Ashukuriwe M/mungu kwa neema hii” aliandika
kabla ya kujinga na WCB, amewahi kushiriki shindano ya kusaka vipaji vya muziki barani Afrika mwaka 2016 liitwalo Tecno Own The Stage ambalo pia  Nandy  alishiriki na kupata Sh36 milioni baada ya kuwa mshindi wa pili.

Pia Zuchi ameshiriki baadhi ya nyimbo ukiwemo ule wa ‘Super Woman’ ambao ulishirikisha wasanii mbalimbali wa kike wa Bongo Fleva na taarabu.
Hata hivyo katika kusaka kipaji chake na kufikia ndoto aliwahi kurudia baadhi ya nyimbo za wasanii madharani wimbo wa Nadekezwa wa msanii Mbosso.

Taarifa zaidi zinasema kuwa Zuchu alikuwa katika lebo hiyo kwa mda mrefu tangu 2018 ambapo amekuja kusainiwa rasmi aprili 8, 2020 Mungu amuongoze katika safari yake ya muziki.






KING KIBA AFUNGUKA UKWELI KUHUSU MOBETTO 

Nyota wa muziki nchini, Ali Salehe ‘King Kiba’ amefunguka na kueleza uhusiano uliopo kati yake na mrembo, Hamisa Mobetto na kusema kuwa anamchukulia  kama msichana anayemuheshimu na anampenda.

“Mimi na Hamisa ni kama familia na mheshimu ni mschina ambaye anajiheshimu na nampenda” alisema Alikiba

Aidha April 8 mwaka huu msanii huyo ametoa wimbo wake mpya uitwao ‘Dodo’ ambapo Hamis ni vixen wa video hiyo.