FIGHT FOR FREEDOM

FIGHT FOR FREEDOM

Kifo cha Otto Warmbier: Trump aishutumu Korea Kaskazini








Rais wa Marekani Donald Trump ameutaja utawala wa taifa la Korea Kaskazini kuwa wa kikatili kufuatia kifo cha mwanafunzi mmoja wa Marekani ambaye alikuwa amefungwa jela kwa zaidi ya miezi 15 nchini humo.
Korea Kaskazini ilimrudisha nyumbani Marekani, Otto Warmbier mwenye umri wa miaka 22 wiki iliopita ikisema kuwa alikuwa hana fahamu kwa kipindi cha mwaka mmoja na kwamba ilikuwa ikimsaidia kibinaadamu.
Wazazi wake wanasema kuwa aliteswa vibaya.

 Bwana Warmbier ambaye alifungwa kwa kujaribu kuiba bango la propaganda kutoka kwa hoteli moja hakuweza kupata fahamu tena.





Bwana Warmbier ambaye alifungwa kwa kujaribu kuiba bango la propaganda kutoka kwa hoteli moja hakuweza kupata fahamu tena.

Wazazi wa Warmbier Fred na Cindy walisema katika taarifa kwamba mwanao alifariki siku ya Jumatatu katika hospitali ya Cincinnati ambapo alikuwa akipewa matibabu.
Wanasema kwamba wakati Otto aliporudi Cincinnati alikuwa hawezi kuzungumza na hakuweza kuona.