Sunday 25 August 2024

MAFURIKO YAUWA WATU 7 INDONESIA

 


WATU 13 wameuwawa na wengine hawajulikani walipo kwenye jimbo la Maluku Kaskazini mwa Indonesia baada ya mafuriko makubwa kulikumba eneo la mashariki mwa visiwa hivyo.

Shirika la utafutaji na uokoaji la Indonesia Basarnas lilisema kwamba mvua kubwa ilionyesha tangu jana Jumamosi ilisababisha mafuriko makubwa katika kisiwa cha Ternate na kwamba kikosi cha uokoaji bado kinaendeleza juhudi za kuwaondoa waathiriwa.

Vyombo vya habari nchini humo viliripoti kwamba watu 11 wamefariki kufuatia mkasa huo lakini afisa wa shirika la Basarnas hakuthibitisha idadi hiyo ya vifo. 

Itakumbukwa kuwa mnamo mwezi Mei takriban watu 60 waliuwawa kutokana na mafuriko na maporomoko ya matope katika mkoa wa Sumatra magharibi mwa Indonesia.


No comments:

Post a Comment

nice