Zipo sababu mbalimbali zinazopelekea wakina mama wengi kushindwa kuzalisha maziwa mengi kwa ajili ya kuwanyonyesha watoto zao. Hata hivyo kama wewe ni mama na una tatizo hilo basi unatakiwa kufanya yafuatayio ili utengeneze maziwa kwa wingi;
1. Nyonyesha mara kwa mara.Nyonyesha angalau mara nane kwa siku. Kadri unavyonyonyesha, ndivyo utatengeneza maziwa zaidi.
2.Tumia vinywaji vya kutosha na kula zaidi.
Epuka kukosa mlo wowote wa siku.
3. Pumzika mara kwa mara.Iwapo baba na
wanafamilia wengine watasaidia na kazi zingine za nyumbani, mama atamhudumia
mtoto vizuri zaidi.
4. Hakikisha maziwa yametoka yote wakati wa
kunyonyesha au unapokamua. Usiache maziwa yako kujaa kwa muda mrefu. Hata kama
uko mbali na mtoto hakikisha unakamua maziwa.
5. Hakikisha mtoto amenyonya maziwa yote mara
mbili kila unaponyonyesha
6. Kwa kina mama ambao hawana maziwa ya kutosha
wanaweza kuongea na daktari akawaandikia dawa za kusaidia kuzalisha maziwa.
No comments:
Post a Comment
nice